Thursday, August 31, 2017

KIATU CHA SULTAN RASMI SOKONI

Mshindi wa "Big Brother Africa" Idriss Sultan kijana kutoka Tanzania ambaye ni mchekeshaji, mtangazaji wa choice Fm radio na pia ni Mjasiliamali anayekuja kwa kasi, na imedhihirika jana baada ya kuzindua bidhaa yake ya Viatu inayoitwa SULTAN SHOES. Viatu hivi vimetengenezwa katika nchi za Ulaya na Asia. Bei zake si kubwa sana zinaendana na hali halisi ya uchumi wa Tanzania. Vitapatikana kwa bei ya shilingi 150,000/= hadi shilingi 300,000/= nchini kote. Kwa sasa hakuna duka maalum ambalo litauza viatu hivi, bali Vitapatikana ONLINE (mtandaoni) ambako utachagua bidhaa yako na kufanya malipo kisha bidhaa utaletewa mpaka mlangoni. Zifuatazo ni baadhi ya picha za viatu hivyo Bidhaa hizi zitapatikana kwenye IG yake inayojulikana kama "Sultan". Hongera nyingi ziende kwake Idriss Sultan kwa kuona fursa na kuifanyia kazi na hii iwe changamoto kwako mtanzania mwenzangu, acha UOGA amka sasa utoke kijasiliamali. Kwa habari za kijasiliamali na nyingine nyingi zinazogusa maisha yako please tembelea blog yetu hii au pakua application yetu ya SAYARINEWZ APPambayo ipo GOOGLE PLAYSTORE ipakue sasa ili usiwe nyuma kupata habari mbalimbali za ujasiriamali.


EmoticonEmoticon